Watu watatu wamelazwa katika Hospitali Kuuu ya Mnazimmoja mjini
Zanzibar baada ya kushukiwa kuwa na maradhi ya homa ya Dengue
inayosababishwa na mbu aina ya “Aedes”Ugonjwa huo tayari umeingia jijini Dar es Salaam na kuathiri watu zaidi ya 400 huku wengine wakiripotiwa
kufariki.Akizungumza na waandishi wa habari visiwani hapa, Waziri wa Afya,
Juma Duni Haji, alisema, wagonjwa hao wametokea katika maeneo ya vijiji
vya Kama na Mwera.Alisema, tokea wagonjwa hao wabainike, uongozi wa Hospitali Kuu ya
Mnazimmoja umeamua kuchukua vipimo kwa ajili ya kuvifanyia uchunguzi
zaidi, ikiwa ni hatua ya kuweza kupata uthibitisho wa wagonjwa hao kama
wanaugua homa hiyo.“Serikali kupitia Wizara ya Afya imeanza kuchukua hatua mbalimbali
ikiwemo kuchukua vipimo (Sample) ili kuchunguza kuwepo kwa virusi hivyo
na kufuatilia sehemu walikotoka wagonjwa ili kutathmini hali halisi ya
mazingira”, alisema Waziri huyo
Waziri Duni, alisema, wanalazimika kuchukua hatua hiyo kwa vile
maradhi hayo ni mara ya kwanza kujitokeza hapa Zanzibar, hivyo ni vyema
wananchi wakaona umuhimu wa kusafisha mazingira yanayowazunguka.Aidha, alifahamisha kuwa hadi sasa hakuna tiba maalum ya ugonjwa huo,
na kwamba mgonjwa anatibiwa kutokana na dalili zitakazoambatana kama
vile homa, kupungukiwa na maji au damu huku akisisitiza hakuna chanjo
kwa ajili ya kingaWaziri Duni, alisema katika kukabiliana na ugonjwa huo, serikali hivi
sasa, inawasiliana na mashirika mbalimbali ya kimataifa ili yaweze
kuwasaidia katika kuleta vifaa vya uuguzi kwa wagonjwa watakaopatwa na
tatizo hilo.
Aliyataja mashirika ambayo wameanza kuwasiliana nayo ni pamoja na WHO, NIMR na Wizara ya Afya Tanzania Bara.
Alizitaja dalili za ugonjwa huo ni homa ya
hafla,mwili kuchoka, kuumwa na viungo, kuvimba tenzi na kupatwa na
haraha (Vipele), kuumwa na kichwa ambapo dalili zake huanza kujitokeza
kuanzia kati ya siku tatu na 14 tangu mtu alipoambukizwa.
“Dalili za ugonjwa huu zinaweza kufanana sana na dalili za malaria na
homa ya mafua, hivyo nawaomba wananchi kuwa waangalifu hasa wakati
wanapopata homa ambazo zinafanana na malaria kukimbilia vituo vya afya,”
alisema.
Hata hivyo, alifahamisha kuwa kuna aina tofauti za ugonjwa huo,
ikiwemo (Dengue Fever) ambapo huambatana na dalili kuu tatu za homa kali
ghafla, kuumwa kichwa na maumivu ya viungo au uchovu.
Dk. Salma Masauni Yussuf, ambae ni Mkuu wa Kitengo cha kuzuia na
kudhibiti maradhi Zanzibar, aliwataka wananchi kushirikiana kwa pamoja
ili kuhakikisha hali inakuwa nzuri hapa nchini huku akiwanasahi
kusafisha mazingira hasa katika kipindi hichi cha mvua za masika
zinazoendelea.
No comments:
Post a Comment