Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), limepatiwa gari jipya la
kisasa la kurushia matangazo ya nje (OB Van), ambalo kwa mara ya kwanza
litatumiwa kwenye matangazo ya sherehe za miaka. 50 ya Muungano wa
Tanzania kesho kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Gari hilo kutoka Serikali ya China limeshawasili
na tayari mafundi tisa wa Kichina wapo nchini ili kusaidia katika
urushaji wa matangazo hayo ya sherehe za Muungano pamoja na kuendesha
mafunzo kwa mafundi wa TBC.Kundi la mafundi wa TBC lilikwenda China wiki
chache zilizopita kujifunza jinsi ya kutumia gari hilo ambalo limeelezwa
kuwa bora kwa kurushia matangazo ya televisheni ya nje kuliko jingine
lolote hapa nchini kwa sasa.Ofisa mwandamizi wa TBC1 ambaye hakutaka jina lake
litajwe alisema ili kukidhi matakwa ya matumizi ya gari hilo, shirika
lao limewajibika kununua gari jingine jipya (pick up) lenye thamani ya
Sh60 milioni kwa ajili ya kubebea mtambo rasmi wa gari hilo wa kurushia
matangazo yake hayo.Alisema sherehe rasmi za uzinduzi na makabidhiano
ya gari hilo zitafanywa baada ya kumalizika kwa shughuli za sherehe za
Muungano.

No comments:
Post a Comment